Translate

Miss Anonymous.

                      

Nikiwasho pahali nilipatana na huyu hamtaamini, the same way sikuamini story alikuwa ananichapia, karibu nimsho heri angekuja na taxin tuchane akinichapia hizo story zake. Alikuwa amekuja kunitembelea nikiwa ndani,  behind bars for a few hours ndio anichapie story nitawachapia in a few. 

Ilikuwa a good day, nilikuwa tu nimetoka site kazi, foreman akiwa amenikanja  zangu after koroga kuisha na sijainama lunch hio siku. Nimeingia pale kejani, nikapiga shower, baadaye ka luku kidogo kutokea streets kutafuta rada ya kesho.  Naenda kuvuka hivi barabara, nduthi inapita shwaa! Karibu ipite na mimi. Nikienda kucheki rada ka ni safi kwa barabara ndio nivuke, nacheki someone's daughter ameivaa! Macho zetu na someone's daughter zikakutana, mimi huyo, nimepiga wink, akasmile, 

green light ukipewa, unaenda huendi?




Confidence iko on, full swing, nikaenda nikajitambulisha, nikamuuliza jina but sitawaambia ju mnaweza fanya ile kitu bana, huwa siwaoni vizuri nyinyi. Jokes kidogo kidogo na kudrop hint kwake that nimechoka ka punda za pipeline. Nastukia tu, pap nimeinvitiwa supper but ka siwezi mind naweza nunua vitu za kupika. Mimi si mind, mfuko saa hio imefura ka tumbo ya your favorite politician.


Tunastep na yeye hadi tu her place, pace tu iko moss moss.  Tukiwa kwa njia, tukastop kwa Pedi, tukishuka stairs ndio tushike njia ya kuelekea kwa dame nastukia msee amenishika haga na kuisqueeze. Venye ngumi ilidescend from the heavens na uzito,  huyo msee alidunda ka gunia ya viazi kutoka Timboroa ikishukishwa kwa lorry. Unacheza na mkono ya mtu yuko juakali..? Sura ya hio msee ilikuwa tu ma dents tu. Huyo msee aliona ni ka aliona nitamuua, venye alijiinua kutoka chini akatoka mbio, weeeh. 


Kumbe watu hawapendi kifo.

😅😅

Mimi huyo nyuma yake, hasira zimenipanda nikimwona war, nataka kumwahi ngumi za mwisho. Akikimbia tu hivi, akafaint mbele ya makarao fulani walikuwa wanapiga patrol. Mimi nikageuka ndio nihepe nikasikia tu 


“Simama..!”

“Unadhani uko na mbio kuliko risasi?”

Shiet kumbe wameniona? Kuna tu situations zingine, inabidi usalimu amri, nikakuwa led away na pingu ka mbuzi kichinjioni. Nimewekwa pingu na escortiwa tu nijibie mastaka mbele ka ule G wa Mau Mau, Dedan Kimathi.  Nikienda kuingia station, nikaona  Dem huko nyuma ananifuata na ujanja. The next day, akiniletea kitu ya kudishi ju nililala cell na hakuna kitu nilikuwa nimekula na ndio alinichapia hii story.

Comments